Lebo

25/09/2016

KUKUA KATIKA KRISTO






Jinsi Yesu alivyokuwa kwa wanafunzi wake katika mambo yote, ndivyo
anavyotaka kuwa kwa watoto wake leo; kwa maana katika sala yake ile ya mwisho,
akiwa na kikundi kidogo cha wanafunzi wake kilichokusanyika pale na kumzunguka,
alisema, “Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya
neno lao.” Yoh. 17:20.
Yesu alituombea sisi, tena aliomba kwamba tupate kuwa umoja naye, kama yeye alivyo umoja na Baba yake. Ni muungano ulioje huo! Kumhusu yeye mwenyewe Mwokozi alisema, “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe, ila lile ambalo amwona Baba analitenda.” “Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.” Yoh. 5:19; 14:10. Basi kama Kristo anakaa ndani ya mioyo yetu, atafanya kazi ndani yetu “kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.” Wafilipi 2:13. Tutafanya kama alivyofanya yeye; tutakuwa na nia ile ile. Na hivyo, tukiendelea kumpenda na kukaa
ndani yake, tuta“kua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, ndiye Kristo.” Efe. 4:15.

Furaha gani na ushiriki,
Nikimtegemea Yesu tu!
Baraka gani, tena amani,
Nikimtegemea Yesu tu!
Tegemea,

Salama bila hatari;
Tegemea,
Tegemea Mwokozi Yesu.

Nitaiweza njia nyembamba,
Nikimtegemea Yesu tu;
Njia ‘tazidi kuwa rahisi,
Nikimtegemea Yesu tu.

Sina sababu ya kuogopa,
Nikimtegemea Yesu tu;
Atakuwa karibu daima,
Nikimtegemea Yesu tu.

(Nyimbo za Kristo, Na. 43)

MWISHO WA SOMO LA KUKUA KATIKA KRISTO BARIKIWA NA MASOMO MENGINE YATAKAYO FUATA.