Lebo

08/08/2015

KUTUBU - 4


Sala ya Daudi baada ya kuanguka kwake dhambini inatudhihirishia vizuri jinsi huzuni ya kweli kwa ajili ya dhambi ilivyo hasa. Kutubu kwake kulikuwa kwa kweli na kwenye kina. Hapakuwa na
jitihada yo yote ya kupunguza ukubwa wa makosa yake; hakuwa na tamaa yo yote ya kuikwepa hukumu iliyotishiwa juu yake ambayo iliivuvia sala yake. Daudi aliuona ukubwa upitao kiasi wa kosa lake; aliona unajisi wa moyo wake; aliichukia sana dhambi yake. Hakuomba ili apate msamaha tu, aliomba pia ili awe na moyo safi. Alitamani sana kuwa na furaha iletwayo na utakatifu - yaani,
kurejeshwa katika hali ya amani na ushirika na Mungu. Hii ilikuwa ndiyo lugha ya roho
yake:


Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake.  Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila.” Zaburi 32:1-2. “Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu. Na dhambi yangu i mbele yangu daima Unioshe nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.

 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu. Usinitenge na uso wako, Wala Roho wako Mtakatifu usiniondolee. Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi, Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu, Utuponye na damu za watu Na ulimi wangu utaiimba haki yako.” Zaburi 51:1-14. Kutubu kwa namna hii hakuwezekani kwetu sisi kwa uwezo wetu wenyewe; kunawezekana katika Kristo tu, aliyepaa juu na kuwapa wanadamu vipawa.

Waliopewa Kitabu - 1

Aya hizi ni NUKUU  kutoka DivineIslam’s Qur’an Viewer software v2.913


Assalamu’ alaikum! Kurani Tukufu huelekeza kidole chake kwenye kundi lile liitwalo “Waliopewa Kitabu”. Msomaji anaombwa asome Sura 3:113-115. Aali Imran. 003:113 “Wao (Waliopewa Kitabu) si wote sawa. Katika (hao) Waliopewa Kitabu wamo watu waliotengenea  wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu (yaani wamesilimu).” 003:114 “Wanamwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na wanaamrisha mema na wanakataza maovu na wanayaendea mbio mambo mema.

Na hao ndio miongoni mwa hao watendao mema (kweli kweli).” 003:115 “Na heri yo yote watakayoifanya hawatakanushiwa (thawabu zake). Na Mwenyezi Mungu anawajua wanaomcha (wakajiepusha na makatazo yake na wakafanya maamrisho yake).” 


 Watu hao wanajulikana kama ‘Wakristo’. Hao wanaitwa ‘Waliopewa Kitabu’ (Maandiko ya Biblia). Lakini miongoni mwao limo kundi la pekee. Kurani Tukufu yasema kwamba ipo tofauti kati ya hao ‘Wakristo’ na ya kwamba ‘si wote sawa.’

Je, kundi hilo la pekee ni akina nani ambao Nabii Muhammad (jina lake na liheshimiwe) alivuta mawazo ya watu kuelekea kwao kwa namna ya ajabu kama hiyo, ya kuwa wao ni ‘miongoni mwa hao watendao mema kweli kweli’! Hebu zingatia tabia zinazolitambulisha kundi hili la pekee kutoka katika Sura 3:113-115
 

1. si (Wakristo) wote sawa
 

2. katika (hao) waliopewa Kitabu wamo watu waliotengenea
 

3. wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu
 

4. wanasujudu
 

5. wanamwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho
 

6. wanaamrisha mema [wanafundisha kwa mamlaka yaliyo ya haki]
 

7. wanakataza maovu
 

8. wanayaendea mbio mambo mema [wanajitahidi kufanya yale yenye sifa njema]
 

9. hao ndio miongoni mwa hao watendao mema kweli
kweli
 

10. na heri yo yote watakayoifanya hawatakanushiwa. [Mwenyezi Mungu anawajua]