The planet EARTH and its relity
Basi mtiini Mungu.Mpingeni Shetani,naye atawakimbia Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi,na kuishafisha mioyo yenu,enyi wenye nia mbili{Yakobo 4:7-8} Submit yourselves then, to God, Resist the devil,and he will flee from you.come near to God and he will. come near you.wash your hands you sinners and purify your hearts you double minded.{James 4:7-8}NIV
08/12/2016
Letters to Young Lovers
Marriage a foretaste of Heaven
Section one.........
The warmth of true friendship and the love that binds the hearts of husband and wife are a
foretaste of heaven. God has ordained that there should be perfect love and perfect harmony between those who enter into the marriage relation.
Let bride and bridegroom in the presence of the heavenly universe pledge themselves to love
one another as God has ordained they should.In Heavenly Places, 202.
A Foretaste of Heaven
Man was not made to dwell in solitude; he was to be a social being. Without companionship the beautiful scenes and delightful employments of Eden would have failed to yield perfect happiness. Even communion with angels could not have satisfied his desire for sympathy and companionship. There was none of the same nature to love and to be loved.
God himself gave Adam a companion. He provided “an help meet for him”a helper corresponding to him one who was fitted to be his companion, and who could be one with him in love and sympathy. Eve was created from a rib taken from the side of Adam, signifying that she was not to control him as the head, nor to be trampled under his feet as an inferior, but to stand by his side as an equal, to be loved and protected by him. A part of man, bone of his bone, and flesh of his flesh, she was his second self, showing the close union and the affectionate attachment that should exist in this relation. “For no man ever yet hated his own flesh; but nourisheth and cherisheth it.” Ephesians 5:29. “Therefore shall a man leave his father and his mother, and shall cleave unto his wife; and they shall be one.” God celebrated the first marriage. Thus the institution has for its originator the Creator of the
universe. “ Marriage is honorable”
(Hebrews 13:4); it was one of the first gifts of God to man, and it is one of the two institutions that,
after the Fall, Adam brought with him beyond the gates of Paradise. When the divine principles
are recognized and obeyed in this relation, marriage is a blessing; it guards the purity and happiness of the race, it provides for man’s social needs, it elevates the physical, the intellectual,
and the moral nature. as the Creator joined the hands of the holy pair [Adam and Eve] in wedlock, saying, A man shall “leave his father and his mother and shall cleave unto his wife; and they shall be one” (Genesis 2:24), He enunciated for all the children of Adam.
That which the Eternal Father Himself had pronounced good was the law of highest blessing
and development for man.”
It is written...........!
“And the dragon was wroth with the woman,
and went to make war with the remnant of
her seed, which keep the commandments of
God, and have the testimony of Jesus.”
—Revelation 12:17
and went to make war with the remnant of
her seed, which keep the commandments of
God, and have the testimony of Jesus.”
—Revelation 12:17
02/12/2016
Kujifunza Kuomba Maombi ya Kweli
SEHEMU YA TATU.
Tunapomwendea Mungu kumwomba rehema zake na mbaraka wake, ingetupasa kuwa na roho ya upendo ndani ya mioyo yetu wenyewe. Twawezaje kuomba hivi, “Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu,” wakati sisi katika roho zetu tungali hatujakubali kuwasamehe wengine. Tukitumaini kujibiwa maombi yetu, sharti tuwe na roho ya kuwasamehe wengine kwa njia ile ile, na kwa kiwango kile kile, kama sisi tunavyotarajia kusamehewa.
Kudumu katika maombi ni sharti jingine lililowekwa ili tupate kupokea.Yatupasa kuomba sikuzote, kama tunataka kukua katika imani na katika uzoefu wa maisha yetu. “Katika kusali, mkidumu,” “dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani.” Rum. 12:12; Kol. 4:2. Petro awausia Wakristo, “Iweni na akili, mkeshe katika sala.” 1 Petro 4:7. Mtume Paulo awaagiza hivi, “Katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane kwa Mungu.” Flp.4:6. Na Yuda pia asema, “Ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu
sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu, jilindeni katika upendo wa Mungu.” Yuda 20,21. Kuomba bila kukoma ni muungano wa mtu na Mungu usioweza kuvunjika, kiasi kwamba uhai toka kwa Mungu unabubujika na kuingia katika maisha yetu; na kutoka katika maisha yetu usafi wa maisha na utakatifu hububujika na kumrudia Mungu.
Umuhimu upo wa kufanya bidii katika kuomba; usikubali kitu cho chote kikuzuie kuomba fanya kila jitihada kuacha wazi mawasiliano kati ya roho yako na Yesu tafuta kila nafasi kwenda mahali ambapo watu huzoea kuomba wale wanaotaka kushirikiana na Mungu kweli kweli wataonekana kila mara kwenye mkutano wa maombi; watakuwa waaminifu katika kufanya wajibu wao, tena watakuwa na bidii na shauku katika kujipatia manufaa yote wawezayo kupata. Watatumia vizuri kila nafasi wapatayo ili kujiweka mahali wawezapo kupokea mionzi ya nuru kutoka mbinguni.
Sharti tuombe pamoja na watu wa nyumbani; na zaidi ya yote tusiwe wavivu katika kuomba faraghani peke yetu; maana kufanya hivyo ndiyo asili ya uzima wa roho zetu. Ni vigumu kabisa kusitawi kiroho wakati maombi yanapuuzwa. Maombi pamoja na watu wa nyumbani na yale ya watu wengi katika ibada hayatoshi. Hebu mahali pale pa faragha moyo wako na ufunguliwe wazi ili upate kuchunguzwa na jicho lake Mungu.
Maombi ya faragha ya mtu akiwa peke yake yanapaswa kusikilizwa tu na Mungu asikiaye maombi. Hakuna sikio lo lote lenye udadisi linalopaswa kupokea mzigo wa dua kama hizo. Katika maombi hayo ya siri mtu hasumbuliwi na mivuto inayomzunguka, hasumbuliwi na misisimko yo yote. Kwa utulivu, lakini kwa dhati, moyo wake unamtafuta Mungu. Mvuto utokao kwake yeye aonaye sirini, ambaye sikio lake li wazi kusikiliza maombi yatokayo moyoni, utakuwa mtamu na wa kudumu. Kwa imani tulivu, ya kawaida, mtu huyo anaongea na Mungu, na kujikusanyia mionzi ya nuru itokayo kwa Mungu inayomtia nguvu na kumtegemeza katika mapambano yake na Shetani. Mungu ni mnara wa nguvu zetu. Omba katika chumba chako cha siri; na unapokwenda kufanya kazi zako za kila siku, umwinulie Mungu moyo wako mara kwa mara. Hivyo ndivyo Henoko alivyopata kutembea pamoja na Mungu. Maombi hayo ya kimya kimya hupanda juu kama uvumba wa thamani kwenda mbele ya kiti cha neema. Shetani hawezi kamwe kumshinda yule ambaye moyo wake humtegemea Mungu hivyo.
Hakuna wakati wala mahali pasipofaa kumwomba Mungu. Hakuna kinachoweza kutuzuia tusimwinulie mioyo yetu tukiwa na roho ya maombi ya dhati. Tukiwa katika makundi ya watu mitaani, katikati ya shughuli zetu za kazi, tunaweza kupeleka dua zetu kwa Mungu, na kumwomba atupe uongozi wake, kama alivyoifanya Nehemia alipotoa ombi lake mbele ya Mfalme Artashasta. Chumba cha siri cha mawasiliano kinaweza kupatikana po pote tulipo. Mlango wa moyo wetu ungefunguliwa wazi daima, na mwaliko wetu ungepanda juu ili Yesu aje na kukaa ndani ya moyo wetu kama mgeni atokaye mbinguni.
Tunapomwendea Mungu kumwomba rehema zake na mbaraka wake, ingetupasa kuwa na roho ya upendo ndani ya mioyo yetu wenyewe. Twawezaje kuomba hivi, “Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu,” wakati sisi katika roho zetu tungali hatujakubali kuwasamehe wengine. Tukitumaini kujibiwa maombi yetu, sharti tuwe na roho ya kuwasamehe wengine kwa njia ile ile, na kwa kiwango kile kile, kama sisi tunavyotarajia kusamehewa.
Kudumu katika maombi ni sharti jingine lililowekwa ili tupate kupokea.Yatupasa kuomba sikuzote, kama tunataka kukua katika imani na katika uzoefu wa maisha yetu. “Katika kusali, mkidumu,” “dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani.” Rum. 12:12; Kol. 4:2. Petro awausia Wakristo, “Iweni na akili, mkeshe katika sala.” 1 Petro 4:7. Mtume Paulo awaagiza hivi, “Katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane kwa Mungu.” Flp.4:6. Na Yuda pia asema, “Ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu
sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu, jilindeni katika upendo wa Mungu.” Yuda 20,21. Kuomba bila kukoma ni muungano wa mtu na Mungu usioweza kuvunjika, kiasi kwamba uhai toka kwa Mungu unabubujika na kuingia katika maisha yetu; na kutoka katika maisha yetu usafi wa maisha na utakatifu hububujika na kumrudia Mungu.
Umuhimu upo wa kufanya bidii katika kuomba; usikubali kitu cho chote kikuzuie kuomba fanya kila jitihada kuacha wazi mawasiliano kati ya roho yako na Yesu tafuta kila nafasi kwenda mahali ambapo watu huzoea kuomba wale wanaotaka kushirikiana na Mungu kweli kweli wataonekana kila mara kwenye mkutano wa maombi; watakuwa waaminifu katika kufanya wajibu wao, tena watakuwa na bidii na shauku katika kujipatia manufaa yote wawezayo kupata. Watatumia vizuri kila nafasi wapatayo ili kujiweka mahali wawezapo kupokea mionzi ya nuru kutoka mbinguni.
Sharti tuombe pamoja na watu wa nyumbani; na zaidi ya yote tusiwe wavivu katika kuomba faraghani peke yetu; maana kufanya hivyo ndiyo asili ya uzima wa roho zetu. Ni vigumu kabisa kusitawi kiroho wakati maombi yanapuuzwa. Maombi pamoja na watu wa nyumbani na yale ya watu wengi katika ibada hayatoshi. Hebu mahali pale pa faragha moyo wako na ufunguliwe wazi ili upate kuchunguzwa na jicho lake Mungu.
Maombi ya faragha ya mtu akiwa peke yake yanapaswa kusikilizwa tu na Mungu asikiaye maombi. Hakuna sikio lo lote lenye udadisi linalopaswa kupokea mzigo wa dua kama hizo. Katika maombi hayo ya siri mtu hasumbuliwi na mivuto inayomzunguka, hasumbuliwi na misisimko yo yote. Kwa utulivu, lakini kwa dhati, moyo wake unamtafuta Mungu. Mvuto utokao kwake yeye aonaye sirini, ambaye sikio lake li wazi kusikiliza maombi yatokayo moyoni, utakuwa mtamu na wa kudumu. Kwa imani tulivu, ya kawaida, mtu huyo anaongea na Mungu, na kujikusanyia mionzi ya nuru itokayo kwa Mungu inayomtia nguvu na kumtegemeza katika mapambano yake na Shetani. Mungu ni mnara wa nguvu zetu. Omba katika chumba chako cha siri; na unapokwenda kufanya kazi zako za kila siku, umwinulie Mungu moyo wako mara kwa mara. Hivyo ndivyo Henoko alivyopata kutembea pamoja na Mungu. Maombi hayo ya kimya kimya hupanda juu kama uvumba wa thamani kwenda mbele ya kiti cha neema. Shetani hawezi kamwe kumshinda yule ambaye moyo wake humtegemea Mungu hivyo.
Hakuna wakati wala mahali pasipofaa kumwomba Mungu. Hakuna kinachoweza kutuzuia tusimwinulie mioyo yetu tukiwa na roho ya maombi ya dhati. Tukiwa katika makundi ya watu mitaani, katikati ya shughuli zetu za kazi, tunaweza kupeleka dua zetu kwa Mungu, na kumwomba atupe uongozi wake, kama alivyoifanya Nehemia alipotoa ombi lake mbele ya Mfalme Artashasta. Chumba cha siri cha mawasiliano kinaweza kupatikana po pote tulipo. Mlango wa moyo wetu ungefunguliwa wazi daima, na mwaliko wetu ungepanda juu ili Yesu aje na kukaa ndani ya moyo wetu kama mgeni atokaye mbinguni.
01/12/2016
Kujifunza Kuomba Maombi ya Kweli
SEHEMU YA PILI.
Giza la Shetani huwafunika wale wanaoacha kuomba. Majaribu ya adui huyo anayonong’ona masikioni mwao huwashawishi wafanye dhambi; na hayo yote ni kwa sababu wao hawazitumii haki zote alizowapa Mungu katika mpango wa mbinguni wa maombi aliowawekea. Kwa nini wana na binti zake Mungu ni wazito sana kuomba,
wakati maombi ni ufunguo katika mkono wa imani uifunguao ghala ya mbinguni, ambamo zimewekwa hazina za msaada na mibaraka isiyo na mwisho ya Mungu mwenye uweza wote? Tusipoomba bila kukoma na kukesha kwa bidii, tutakuwa katika hatari ya kutojali na kukengeuka kutoka katika njia ile ya haki. Adui hutafuta daima kuzuia njia iendayo kwenye kiti cha rehema, ili kwa maombi ya dhati na imani tusiweze kupokea neema na nguvu ya kutusaidia kuyapinga majaribu.
Kuna masharti fulani ambayo yakitimizwa Mungu anaweza kutazamiwa kusikia na kujibu maombi yetu. La kwanza katika hayo ni kwamba sisi tutambue kwamba tunahitaji msaada wake. Yeye ameahidi, amesema, “Nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu.” Isa. 44:3. Wale walio na njaa na kiu ya haki, wanaomtamani sana Mungu, wawe na hakika kwamba watashibishwa.
Ni lazima moyo ufunguliwe kupokea mvuto wa Roho, vinginevyo, mbaraka wa Mungu hauwezi
kupokewa. Haja yetu kuu kwa yenyewe ndiyo hoja yetu, nayo inatuombea sisi kwa ufasaha kabisa. Lakini sisi hatuna budi kumtafuta Bwana ili apate kutufanyia mambo hayo. Asema, “Ombeni, nanyi mtapewa.” Mathayo 7:7. Tena “Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye.” Warumi 8:32. Kama tunawaza maovu mioyoni mwetu, kama tunaing’ang’ania dhambi yoyote tuijuayo, Bwana hatatusikia; lakini sala ya mtu yule aliyetubu, na kupondeka moyo wake, inakubaliwa daima. Makosa yote tunayoyajua yanaposahihishwa, tunaweza kusadiki ya kwamba Mungu atazijibu dua zetu. Wema wetu wenyewe hauwezi kamwe kutupatia sifa za kupewa upendeleo wa Mungu; ni ustahilifu wa Yesu utakaotuokoa sisi, ni damu yake ndiyo itakayotutakasa; hata hivyo tunayo kazi ya kufanya katika
kuyatimiza masharti ya kukubaliwa naye.
Sharti jingine la maombi yanayopata ushindi ni kuwa na imani. “Pasipo imani haiwezekani kumpendeza (Mungu): kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Ebr. 11:6. Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” Marko 11:24. Je, twayasadiki maneno yake?
Ahadi hiyo ni pana, tena haina mipaka, na yule aliyeahidi ni mwaminifu. Tusipopokea mambo yale yale tuliyoyaomba kwa wakati ule ule tuombao, bado yatupasa kuamini kwamba Bwana wetu anatusikia, na ya kwamba atajibu maombi yetu. Sisi tunakosea mno, wala hatuoni mbali, hata wakati mwingine tunaomba mambo ambayo yasingekuwa mbaraka kwetu, na Baba yetu aliye mbinguni kwa upendo wake anajibu maombi yetu kwa kutupa kile ambacho kitakuwa kwa manufaa yetu ya kiwango cha juu kabisa yaani, kile ambacho sisi tungekitamani kama macho yetu yangetiwa nuru na
Mungu na tungeweza kuyaona mambo yote kama yalivyo hasa.
Maombi yetu yanapoonekana kana kwamba hayajibiwi, hatuna budi kuishikilia sana ahadi hiyo; kwa maana wakati wa kujibu utakuja hakika, nasi tutapokea mbaraka ule tunaouhitaji sana. Lakini kudai kwamba maombi yetu sikuzote yatajibiwa kwa njia ile ile hasa na ya kwamba tutapewa kitu kile kile hasa tunachokitamani ni ufidhuli. Mungu ni mwenye hekima mno hawezi kufanya kosa, tena ni mwema mno hawezi kuwanyima kitu chochote kilicho chema hao waendao kwa ukamilifu. Basi usiogope kumtegemea yeye, hata kama huoni jibu la mara moja kwa maombi yako. Tegemea ahadi yake hii ya kweli,“Ombeni, nanyi mtapewa.”
Tukishawishiwa na mashaka yetu na hofu zetu, au tukijaribu kupata ufumbuzi kwa kila kitu tusichoweza kukiona waziwazi, kabla hatujawa na imani, matatizo yetu yatazidi kuongezeka na kuwa makubwa zaidi. Lakini tukimwendea Mungu, huku tukijiona kuwa hatuna uwezo kabisa, tena tumekuwa watu wanaotegemea kusaidiwa naye, kama vile tulivyo hasa, kisha kwa unyenyekevu na imani inayomtegemea tunamjulisha, yeye ambaye maarifa yake hayana mipaka, mambo yale tunayotaka, yeye aonaye kila kitu alichokiumba, tena atawalaye vyote kwa mapenzi yake na neno lake, ndipo ataweza, tena atakisikiliza kilio chetu, na kuiangaza nuru yake mioyoni mwetu.
Kwa njia ya maombi yanayotolewa kwa moyo mnyofu tunaunganishwa na mawazo ya Mungu. Huenda tusione ushahidi wo wote wa kustaajabisha wakati uso wa Mkombozi wetu unapoinama chini na kutuangalia kwa huruma na upendo; lakini jambo hilo ndivyo lilivyo hasa. Huenda tusisikie mguso wake unaoonekana kwa macho, lakini mkono wake u juu yetu kuonyesha upendo na huruma yake inayoumia pamoja nasi.
Giza la Shetani huwafunika wale wanaoacha kuomba. Majaribu ya adui huyo anayonong’ona masikioni mwao huwashawishi wafanye dhambi; na hayo yote ni kwa sababu wao hawazitumii haki zote alizowapa Mungu katika mpango wa mbinguni wa maombi aliowawekea. Kwa nini wana na binti zake Mungu ni wazito sana kuomba,
wakati maombi ni ufunguo katika mkono wa imani uifunguao ghala ya mbinguni, ambamo zimewekwa hazina za msaada na mibaraka isiyo na mwisho ya Mungu mwenye uweza wote? Tusipoomba bila kukoma na kukesha kwa bidii, tutakuwa katika hatari ya kutojali na kukengeuka kutoka katika njia ile ya haki. Adui hutafuta daima kuzuia njia iendayo kwenye kiti cha rehema, ili kwa maombi ya dhati na imani tusiweze kupokea neema na nguvu ya kutusaidia kuyapinga majaribu.
Kuna masharti fulani ambayo yakitimizwa Mungu anaweza kutazamiwa kusikia na kujibu maombi yetu. La kwanza katika hayo ni kwamba sisi tutambue kwamba tunahitaji msaada wake. Yeye ameahidi, amesema, “Nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu.” Isa. 44:3. Wale walio na njaa na kiu ya haki, wanaomtamani sana Mungu, wawe na hakika kwamba watashibishwa.
Ni lazima moyo ufunguliwe kupokea mvuto wa Roho, vinginevyo, mbaraka wa Mungu hauwezi
kupokewa. Haja yetu kuu kwa yenyewe ndiyo hoja yetu, nayo inatuombea sisi kwa ufasaha kabisa. Lakini sisi hatuna budi kumtafuta Bwana ili apate kutufanyia mambo hayo. Asema, “Ombeni, nanyi mtapewa.” Mathayo 7:7. Tena “Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye.” Warumi 8:32. Kama tunawaza maovu mioyoni mwetu, kama tunaing’ang’ania dhambi yoyote tuijuayo, Bwana hatatusikia; lakini sala ya mtu yule aliyetubu, na kupondeka moyo wake, inakubaliwa daima. Makosa yote tunayoyajua yanaposahihishwa, tunaweza kusadiki ya kwamba Mungu atazijibu dua zetu. Wema wetu wenyewe hauwezi kamwe kutupatia sifa za kupewa upendeleo wa Mungu; ni ustahilifu wa Yesu utakaotuokoa sisi, ni damu yake ndiyo itakayotutakasa; hata hivyo tunayo kazi ya kufanya katika
kuyatimiza masharti ya kukubaliwa naye.
Sharti jingine la maombi yanayopata ushindi ni kuwa na imani. “Pasipo imani haiwezekani kumpendeza (Mungu): kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Ebr. 11:6. Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” Marko 11:24. Je, twayasadiki maneno yake?
Ahadi hiyo ni pana, tena haina mipaka, na yule aliyeahidi ni mwaminifu. Tusipopokea mambo yale yale tuliyoyaomba kwa wakati ule ule tuombao, bado yatupasa kuamini kwamba Bwana wetu anatusikia, na ya kwamba atajibu maombi yetu. Sisi tunakosea mno, wala hatuoni mbali, hata wakati mwingine tunaomba mambo ambayo yasingekuwa mbaraka kwetu, na Baba yetu aliye mbinguni kwa upendo wake anajibu maombi yetu kwa kutupa kile ambacho kitakuwa kwa manufaa yetu ya kiwango cha juu kabisa yaani, kile ambacho sisi tungekitamani kama macho yetu yangetiwa nuru na
Mungu na tungeweza kuyaona mambo yote kama yalivyo hasa.
Maombi yetu yanapoonekana kana kwamba hayajibiwi, hatuna budi kuishikilia sana ahadi hiyo; kwa maana wakati wa kujibu utakuja hakika, nasi tutapokea mbaraka ule tunaouhitaji sana. Lakini kudai kwamba maombi yetu sikuzote yatajibiwa kwa njia ile ile hasa na ya kwamba tutapewa kitu kile kile hasa tunachokitamani ni ufidhuli. Mungu ni mwenye hekima mno hawezi kufanya kosa, tena ni mwema mno hawezi kuwanyima kitu chochote kilicho chema hao waendao kwa ukamilifu. Basi usiogope kumtegemea yeye, hata kama huoni jibu la mara moja kwa maombi yako. Tegemea ahadi yake hii ya kweli,“Ombeni, nanyi mtapewa.”
Tukishawishiwa na mashaka yetu na hofu zetu, au tukijaribu kupata ufumbuzi kwa kila kitu tusichoweza kukiona waziwazi, kabla hatujawa na imani, matatizo yetu yatazidi kuongezeka na kuwa makubwa zaidi. Lakini tukimwendea Mungu, huku tukijiona kuwa hatuna uwezo kabisa, tena tumekuwa watu wanaotegemea kusaidiwa naye, kama vile tulivyo hasa, kisha kwa unyenyekevu na imani inayomtegemea tunamjulisha, yeye ambaye maarifa yake hayana mipaka, mambo yale tunayotaka, yeye aonaye kila kitu alichokiumba, tena atawalaye vyote kwa mapenzi yake na neno lake, ndipo ataweza, tena atakisikiliza kilio chetu, na kuiangaza nuru yake mioyoni mwetu.
Kwa njia ya maombi yanayotolewa kwa moyo mnyofu tunaunganishwa na mawazo ya Mungu. Huenda tusione ushahidi wo wote wa kustaajabisha wakati uso wa Mkombozi wetu unapoinama chini na kutuangalia kwa huruma na upendo; lakini jambo hilo ndivyo lilivyo hasa. Huenda tusisikie mguso wake unaoonekana kwa macho, lakini mkono wake u juu yetu kuonyesha upendo na huruma yake inayoumia pamoja nasi.
29/11/2016
Kujifunza Kuomba Maombi ya Kweli
SEHEMU YA KWANZA
MUNGU huzungumza nasi kupitia katika viumbe vyake vya asili na mafunuo yake, kupitia katika maongozi yake, na kwa njia ya Roho wake. Lakini njia hizo hazitoshi; sisi pia tunahitaji kumfungulia mioyo yetu. Ili tupate uzima wa kiroho na nguvu yake, hatuna budi kuongea na Baba yetu aliye mbinguni. Mawazo yetu yanaweza kuvutwa kwake; tunaweza kuzitafakari kazi zake, rehema zake, baraka zake; lakini hayo, kwa maana yake kamili, si kuongea naye. Ili tuweze kuongea na Mungu, ni sharti tuwe na mambo fulani ya kumwambia hasa kuhusu maisha yetu tunayoishi.Katika kuomba tunamfunulia Mungu mioyo yetu na kuongea naye kama tunavyoongea na rafiki wa kweli. Si lazima kufanya hivyo ili kumjulisha Mungu hali yetu ilivyo, bali kuongea naye kunatuwezesha kumpokea mioyoni mwetu.
Maombi hayamlazimishi Mungu kushuka kwetu, bali ni sisi ambao tunainuliwa mpaka kufika
kwake. Yesu alipokuwapo hapa duniani, aliwafundisha wanafunzi wake kusali. Aliwaagiza waweke mahitaji yao ya kila siku mbele za Mungu, na kumtwika mizigo yao yote. Na ahadi ile aliyowapa kwamba dua zao zingesikilizwa ni ahadi iliyotolewa kwetu pia. Yesu mwenyewe, alipokaa na wanadamu, aliomba mara nyingi.
Mwokozi wetu alishiriki katika shida zetu na udhaifu wetu; hivyo akawa mhitaji na mwombaji, akimwomba Baba yake ili apate nguvu mpya za kufanya kazi yake na kuwa tayari kupambana na kazi na majaribu yatakayompata. Yeye ndiye mfano wetu katika mambo yote. Ni ndugu yetu ashirikiye udhaifu wetu, “alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote;” lakini kwa sababu alikuwa hana dhambi, aliyaepuka maovu nafsini mwake; alistahimili mapambano na maumivu makali moyoni mwake katika dunia hii yenye dhambi. Ubinadamu wake ulifanya maombi kuwa ya lazima kwake na haki yake.
Alipata faraja na furaha katika kuongea na Baba yake. Na iwapo Mwokozi huyo wa wanadamu, Mwana wa Mungu, aliona kwamba anahitaji kuomba, je! sisi, tulio wanadamu dhaifu wenye dhambi, tusingeona kwamba ni jambo la lazima zaidi kwetu kuomba bila kukoma. Baba yetu aliye mbinguni anangojea kutumwagia baraka zake juu yetu kwa utimilifu. Ni fursa yetu kunywa maji mengi kwenye chemchemi ya pendo lake.
Ni jambo la kushangaza jinsi gani ya kwamba sisi tunaomba kidogo mno! Mungu yu tayari, tena
anapenda kusikiliza maombi ya kweli ya mtoto wake aliye duni kabisa, walakini sisi kwa upande wetu hatuna moyo sana wa kumwambia Mungu haja zetu. Hivi malaika wa mbinguni wanafikirije kuhusu wanadamu maskini wasio na msaada wo wote, ambao wanakabiliwa na majaribu, wakati moyo wa Mungu uliojaa upendo usio na kikomo unapowaonea shauku nyingi sana, akiwa tayari kuwapa zaidi ya yale waombayo au kufikiria, na bado maombi yao ni kidogo sana, tena wana imani ndogo kabisa? Malaika wanapenda kusujudu mbele zake Mungu; wanapenda kuwa karibu naye. Wanaona kwamba maongezi yao na Mungu ni upeo wa furaha yao; lakini watoto wa dunia hii,
wanaohitaji msaada mwingi mno ambao ni Mungu pekee awezaye kuwapa, wanaonekana
kana kwamba wametosheka kutembea bila ya kuwa na nuru ya Roho wake, yaani, ushirika wa kuwako kwake.
Giza la Shetani huwafunika wale wanaoacha kuomba. Majaribu ya adui huyo anayonong’ona masikioni mwao huwashawishi wafanye dhambi; na hayo yote ni kwa sababu wao hawazitumii haki zote alizowapa Mungu katika mpango wa mbinguni wa maombi aliowawekea. Kwa nini wana na binti zake Mungu ni wazito sana kuomba, wakati maombi ni ufunguo katika mkono wa imani uifunguao ghala ya mbinguni, ambamo zimewekwa hazina za msaada na mibaraka isiyo na mwisho ya Mungu mwenye uweza wote? Tusipoomba bila kukoma na kukesha kwa bidii, tutakuwa katika hatari ya kutojali na kukengeuka kutoka katika njia ile ya haki. Adui hutafuta daima kuzuia njia iendayo kwenye kiti cha rehema, ili kwa maombi ya dhati na imani tusiweze kupokea
neema na nguvu ya kutusaidia kuyapinga majaribu.
MUNGU huzungumza nasi kupitia katika viumbe vyake vya asili na mafunuo yake, kupitia katika maongozi yake, na kwa njia ya Roho wake. Lakini njia hizo hazitoshi; sisi pia tunahitaji kumfungulia mioyo yetu. Ili tupate uzima wa kiroho na nguvu yake, hatuna budi kuongea na Baba yetu aliye mbinguni. Mawazo yetu yanaweza kuvutwa kwake; tunaweza kuzitafakari kazi zake, rehema zake, baraka zake; lakini hayo, kwa maana yake kamili, si kuongea naye. Ili tuweze kuongea na Mungu, ni sharti tuwe na mambo fulani ya kumwambia hasa kuhusu maisha yetu tunayoishi.Katika kuomba tunamfunulia Mungu mioyo yetu na kuongea naye kama tunavyoongea na rafiki wa kweli. Si lazima kufanya hivyo ili kumjulisha Mungu hali yetu ilivyo, bali kuongea naye kunatuwezesha kumpokea mioyoni mwetu.
Maombi hayamlazimishi Mungu kushuka kwetu, bali ni sisi ambao tunainuliwa mpaka kufika
kwake. Yesu alipokuwapo hapa duniani, aliwafundisha wanafunzi wake kusali. Aliwaagiza waweke mahitaji yao ya kila siku mbele za Mungu, na kumtwika mizigo yao yote. Na ahadi ile aliyowapa kwamba dua zao zingesikilizwa ni ahadi iliyotolewa kwetu pia. Yesu mwenyewe, alipokaa na wanadamu, aliomba mara nyingi.
Mwokozi wetu alishiriki katika shida zetu na udhaifu wetu; hivyo akawa mhitaji na mwombaji, akimwomba Baba yake ili apate nguvu mpya za kufanya kazi yake na kuwa tayari kupambana na kazi na majaribu yatakayompata. Yeye ndiye mfano wetu katika mambo yote. Ni ndugu yetu ashirikiye udhaifu wetu, “alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote;” lakini kwa sababu alikuwa hana dhambi, aliyaepuka maovu nafsini mwake; alistahimili mapambano na maumivu makali moyoni mwake katika dunia hii yenye dhambi. Ubinadamu wake ulifanya maombi kuwa ya lazima kwake na haki yake.
Alipata faraja na furaha katika kuongea na Baba yake. Na iwapo Mwokozi huyo wa wanadamu, Mwana wa Mungu, aliona kwamba anahitaji kuomba, je! sisi, tulio wanadamu dhaifu wenye dhambi, tusingeona kwamba ni jambo la lazima zaidi kwetu kuomba bila kukoma. Baba yetu aliye mbinguni anangojea kutumwagia baraka zake juu yetu kwa utimilifu. Ni fursa yetu kunywa maji mengi kwenye chemchemi ya pendo lake.
Ni jambo la kushangaza jinsi gani ya kwamba sisi tunaomba kidogo mno! Mungu yu tayari, tena
anapenda kusikiliza maombi ya kweli ya mtoto wake aliye duni kabisa, walakini sisi kwa upande wetu hatuna moyo sana wa kumwambia Mungu haja zetu. Hivi malaika wa mbinguni wanafikirije kuhusu wanadamu maskini wasio na msaada wo wote, ambao wanakabiliwa na majaribu, wakati moyo wa Mungu uliojaa upendo usio na kikomo unapowaonea shauku nyingi sana, akiwa tayari kuwapa zaidi ya yale waombayo au kufikiria, na bado maombi yao ni kidogo sana, tena wana imani ndogo kabisa? Malaika wanapenda kusujudu mbele zake Mungu; wanapenda kuwa karibu naye. Wanaona kwamba maongezi yao na Mungu ni upeo wa furaha yao; lakini watoto wa dunia hii,
wanaohitaji msaada mwingi mno ambao ni Mungu pekee awezaye kuwapa, wanaonekana
kana kwamba wametosheka kutembea bila ya kuwa na nuru ya Roho wake, yaani, ushirika wa kuwako kwake.
Giza la Shetani huwafunika wale wanaoacha kuomba. Majaribu ya adui huyo anayonong’ona masikioni mwao huwashawishi wafanye dhambi; na hayo yote ni kwa sababu wao hawazitumii haki zote alizowapa Mungu katika mpango wa mbinguni wa maombi aliowawekea. Kwa nini wana na binti zake Mungu ni wazito sana kuomba, wakati maombi ni ufunguo katika mkono wa imani uifunguao ghala ya mbinguni, ambamo zimewekwa hazina za msaada na mibaraka isiyo na mwisho ya Mungu mwenye uweza wote? Tusipoomba bila kukoma na kukesha kwa bidii, tutakuwa katika hatari ya kutojali na kukengeuka kutoka katika njia ile ya haki. Adui hutafuta daima kuzuia njia iendayo kwenye kiti cha rehema, ili kwa maombi ya dhati na imani tusiweze kupokea
neema na nguvu ya kutusaidia kuyapinga majaribu.
KUMJUA MUNGU
SOMO LA TATU.
Tusifungue kabisa Biblia na kuyasoma maneno yake bila kuomba. Kabla ya kuzifungua kurasa zake ingetupasa kuomba ufahamu kutoka kwa Roho Mtakatifu, naye atatupa. Nathanaeli alipomwendea Yesu, Mwokozi alisema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.” Nathanaeli akamwambia, “Umepataje kunitambua?”Yesu akajibu, akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini, nilikuona.” Yoh. 1:47,48. Na Yesu atatuona sisi mahali pa siri pa sala, ikiwa tutamwomba ili tupate kuelimishwa na kuyajua yaliyo ya kweli.
Malaika watokao kwenye ulimwengu ule wa nuru watakuwa pamoja na wale ambao kwa unyenyekevu wa moyo wanatafuta uongozi wa Mungu. Roho Mtakatifu humwinua na kumtukuza Mwokozi. Ni kazi yake kutuonyesha Kristo, na hali yake jinsi ilivyo yenye haki na usafi, na kutudhihirishia habari za wokovu mkuu tupatao kwake. Yesu alisema, “Atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasha habari.” Yohana 16:14. Roho wa kweli ndiye mwalimu pekee awezaye kutujulisha
barabara ile kweli ya Mungu. Ni dhahiri kwamba Mungu huwaona wanadamu kuwa wa thamani kubwa, kwa kuwa alimtoa Mwanawe afe kwa ajili yao, tena amemweka Roho
wake kuwa mwalimu na kiongozi wa wanadamu daima.
Nataka nimjue Yesu,
Na nizidi kumfahamu;
Nijue pendo lake tu,
Wokovu wake kamili.
Nataka nione Yesu,
Na nizidi kusikia
Anenapo kitabuni,
Kujidhihirisha kwangu.
Nataka tena zaidi,
Daima kupambanua
Mapenzi yake, nifanye
Yale yanayompendeza.
Nataka nikae naye,
Kwa mazungumzo matamu.
Nizidi kuwaonyesha
Wengine wokovu wake.
Zaidi, zaidi,
Nimfahamu Yesu,
Nijue upendo wake,
Wokovu wake kamili.
Tusifungue kabisa Biblia na kuyasoma maneno yake bila kuomba. Kabla ya kuzifungua kurasa zake ingetupasa kuomba ufahamu kutoka kwa Roho Mtakatifu, naye atatupa. Nathanaeli alipomwendea Yesu, Mwokozi alisema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.” Nathanaeli akamwambia, “Umepataje kunitambua?”Yesu akajibu, akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini, nilikuona.” Yoh. 1:47,48. Na Yesu atatuona sisi mahali pa siri pa sala, ikiwa tutamwomba ili tupate kuelimishwa na kuyajua yaliyo ya kweli.
Malaika watokao kwenye ulimwengu ule wa nuru watakuwa pamoja na wale ambao kwa unyenyekevu wa moyo wanatafuta uongozi wa Mungu. Roho Mtakatifu humwinua na kumtukuza Mwokozi. Ni kazi yake kutuonyesha Kristo, na hali yake jinsi ilivyo yenye haki na usafi, na kutudhihirishia habari za wokovu mkuu tupatao kwake. Yesu alisema, “Atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasha habari.” Yohana 16:14. Roho wa kweli ndiye mwalimu pekee awezaye kutujulisha
barabara ile kweli ya Mungu. Ni dhahiri kwamba Mungu huwaona wanadamu kuwa wa thamani kubwa, kwa kuwa alimtoa Mwanawe afe kwa ajili yao, tena amemweka Roho
wake kuwa mwalimu na kiongozi wa wanadamu daima.
Nataka nimjue Yesu,
Na nizidi kumfahamu;
Nijue pendo lake tu,
Wokovu wake kamili.
Nataka nione Yesu,
Na nizidi kusikia
Anenapo kitabuni,
Kujidhihirisha kwangu.
Nataka tena zaidi,
Daima kupambanua
Mapenzi yake, nifanye
Yale yanayompendeza.
Nataka nikae naye,
Kwa mazungumzo matamu.
Nizidi kuwaonyesha
Wengine wokovu wake.
Zaidi, zaidi,
Nimfahamu Yesu,
Nijue upendo wake,
Wokovu wake kamili.
28/11/2016
KUMJUA MUNGU
SOMO LA PILI.
Jambo kuu la ukombozi ni moja ambalo malaika wanatamani kulichungulia; litakuwa ndiyo sayansi na wimbo wa waliokombolewa milele hata milele. Je, si jambo lifaalo kufikiriwa sana na kuchunguzwa nasi katika siku hizi? Rehema isiyo na kikomo na upendo wa Yesu, kafara iliyotolewa kwa ajili yetu, mambo hayo hututaka sisi tuyatafakari kwa makini na kwa uzito wake.
Tungeongelea sana juu ya tabia ya Mpendwa Mkombozi na Mwombezi wetu. Tungetafakari sana juu ya utume wake yeye aliyekuja kuwaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao. Tukitafakari hivyo juu ya mambo makuu ya mbinguni, imani yetu na upendo wetu vitakua na kuwa na nguvu nyingi zaidi, na maombi yetu yatazidi kukubalika na Mungu, kwa sababu yatakuwa yamechanganyika na imani na upendo kwa wingi zaidi. Yatatolewa kwa akili na kwa dhati. Na tunapowaza mambo matakatifu, imani yetu itaongezeka kwake, na upendo wetu pia, tena kwa ajili hiyo maombi yetu yatazidi kukubaliwa na Mungu. Kuwa na imani na
Yesu kutazidi kuongezeka daima, pamoja na uzoefu hai wa maisha ya kila siku unaoutegemea uweza wake wa “kuwaokoa kabisa wale wote wamjiao Mungu kwa yeye.” Waeb. 7:25. Na tunapotafakari juu ya ukamilifu alio nao Mwokozi, tutatamani kugeuzwa tabia zetu kabisa, na kufanywa upya kufanana naye katika usafi wake. Patakuwa na njaa na kiu ya roho ya kutaka kufanana naye yule tumpendaye sana. Kadiri tunavyozidi kumfikiria zaidi Kristo, ndivyo kadiri tutakavyozidi kuongea habari zake kwa wengine na kumwakilisha ulimwenguni.
Biblia haikuandikwa kwa ajili ya wataalamu wa Biblia peke yao; kinyume chake, ilitayarishwa kwa ajili ya watu wa kawaida. Kweli zile kuu ambazo ni za lazima kwa wokovu zimeelezwa waziwazi kama nuru ya adhuhuri; wala hakuna mtu ye yote awezaye kukosa kuzielewa na kupotea njia isipokuwa ni wale wanaofuata maoni yao wenyewe badala ya mapenzi ya Mungu yaliyofunuliwa wazi.
Tusikubali kupokea ushuhuda wa mtu ye yote juu ya kile Maandiko yafundishacho, ila tujifunze sisi wenyewe maneno hayo ya Mungu. Tukiwaruhusu wengine kufikiri mambo ya Biblia kwa niaba yetu, tutakuwa na nguvu kama ya kiwete na uwezo uliopungua sana nguvu yake. Nguvu bora za akili zetu zinaweza kudumaa mno kwa kukosa mazoezi ya kufikiri juu ya mambo makuu yanayofaa kutafakariwa kiasi cha kuweza kupoteza uwezo wake wa kuelewa maana zenye kina za Neno la Mungu.
Ubongo wetu utapanuka ukitumika kuchunguza uhusiano uliopo kati ya masomo ya Biblia, Maandiko yakilinganishwa na Maandiko, na mambo ya kiroho yakilinganishwa
na mambo ya kiroho.Hakuna njia nyingine iliyokusudiwa kuitia akili nguvu nyingi zaidi kama ile ya
kujifunza na kuyachunguza Maandiko. Hakuna kitabu kingine kilicho na uwezo mkubwa mno wa kuyakuza mawazo yetu, kuzipa nguvu fahamu za ubongo wetu, kama zilivyo hizo kweli pana, ziadilishazo, za Biblia. Kama wanadamu wangejifunza na kulichunguza Neno la Mungu kama inavyostahili, wangekuwa na maarifa mengi na tabia bora, na kuwa na kusudi thabiti ambalo katika nyakati hizi ni shida mno kuliona.
Lakini kuna manufaa kidogo tu yanayopatikana kwa kusoma Maandiko kwa haraka. Mmoja anaweza kuisoma Biblia yote, lakini bado ashindwe kutambua uzuri wake, wala kuelewa maana yake yenye kina iliyojificha. Kujifunza kifungu kimoja cha maneno mpaka maana yake imekuwa dhahiri, na uhusiano wake na mpango wa wokovu unaeleweka wazi, kuna manufaa mengi sana kuliko kuzisoma sura nyingi kwa juu juu tu bila ya kuwa na kusudi lo lote dhahiri wala kupata mafundisho yo yote yanayojenga.
Biblia yako iwe karibu nawe kila mara. Kila upatapo nafasi, isome; jifunze mafungu yake kwa moyo. Hata wakati utembeapo mitaani, waweza kusoma fungu fulani, na kwa njia hiyo kulikaza mawazoni mwako.Hatuwezi kupata hekima bila kujitahidi kwa dhati na kujifunza kwa moyo wa maombi. Baadhi ya sehemu za Maandiko maana yake imekuwa dhahiri kabisa; lakini kuna sehemu nyingine ambazo maana yake si rahisi kufahamika mara moja. Maandiko yanapaswa kulinganishwa na Maandiko mengine. Lazima pawe na utafiti wa makini na kutafakari kwa moyo wa maombi. Na kujifunza kama huko kutapata malipo maradufu. Kama vile mchimba madini anavyogundua mabamba ya mawe ya madini ya thamani yaliyojificha chini ya uso wa nchi, ndivyo yule anayestahimili kulichunguza Neno la Mungu, kama hazina iliyositirika, azionavyo kweli za thamani kuu mno, ambazo zimefichwa asiweze kuziona mtafutaji mzembe. Maneno hayo ya uvuvio, tukiyatafakari mioyoni mwetu, yatakuwa kama vijito vitiririkavyo kutoka katika chemchemi ya uzima.
Jambo kuu la ukombozi ni moja ambalo malaika wanatamani kulichungulia; litakuwa ndiyo sayansi na wimbo wa waliokombolewa milele hata milele. Je, si jambo lifaalo kufikiriwa sana na kuchunguzwa nasi katika siku hizi? Rehema isiyo na kikomo na upendo wa Yesu, kafara iliyotolewa kwa ajili yetu, mambo hayo hututaka sisi tuyatafakari kwa makini na kwa uzito wake.
Tungeongelea sana juu ya tabia ya Mpendwa Mkombozi na Mwombezi wetu. Tungetafakari sana juu ya utume wake yeye aliyekuja kuwaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao. Tukitafakari hivyo juu ya mambo makuu ya mbinguni, imani yetu na upendo wetu vitakua na kuwa na nguvu nyingi zaidi, na maombi yetu yatazidi kukubalika na Mungu, kwa sababu yatakuwa yamechanganyika na imani na upendo kwa wingi zaidi. Yatatolewa kwa akili na kwa dhati. Na tunapowaza mambo matakatifu, imani yetu itaongezeka kwake, na upendo wetu pia, tena kwa ajili hiyo maombi yetu yatazidi kukubaliwa na Mungu. Kuwa na imani na
Yesu kutazidi kuongezeka daima, pamoja na uzoefu hai wa maisha ya kila siku unaoutegemea uweza wake wa “kuwaokoa kabisa wale wote wamjiao Mungu kwa yeye.” Waeb. 7:25. Na tunapotafakari juu ya ukamilifu alio nao Mwokozi, tutatamani kugeuzwa tabia zetu kabisa, na kufanywa upya kufanana naye katika usafi wake. Patakuwa na njaa na kiu ya roho ya kutaka kufanana naye yule tumpendaye sana. Kadiri tunavyozidi kumfikiria zaidi Kristo, ndivyo kadiri tutakavyozidi kuongea habari zake kwa wengine na kumwakilisha ulimwenguni.
Biblia haikuandikwa kwa ajili ya wataalamu wa Biblia peke yao; kinyume chake, ilitayarishwa kwa ajili ya watu wa kawaida. Kweli zile kuu ambazo ni za lazima kwa wokovu zimeelezwa waziwazi kama nuru ya adhuhuri; wala hakuna mtu ye yote awezaye kukosa kuzielewa na kupotea njia isipokuwa ni wale wanaofuata maoni yao wenyewe badala ya mapenzi ya Mungu yaliyofunuliwa wazi.
Tusikubali kupokea ushuhuda wa mtu ye yote juu ya kile Maandiko yafundishacho, ila tujifunze sisi wenyewe maneno hayo ya Mungu. Tukiwaruhusu wengine kufikiri mambo ya Biblia kwa niaba yetu, tutakuwa na nguvu kama ya kiwete na uwezo uliopungua sana nguvu yake. Nguvu bora za akili zetu zinaweza kudumaa mno kwa kukosa mazoezi ya kufikiri juu ya mambo makuu yanayofaa kutafakariwa kiasi cha kuweza kupoteza uwezo wake wa kuelewa maana zenye kina za Neno la Mungu.
Ubongo wetu utapanuka ukitumika kuchunguza uhusiano uliopo kati ya masomo ya Biblia, Maandiko yakilinganishwa na Maandiko, na mambo ya kiroho yakilinganishwa
na mambo ya kiroho.Hakuna njia nyingine iliyokusudiwa kuitia akili nguvu nyingi zaidi kama ile ya
kujifunza na kuyachunguza Maandiko. Hakuna kitabu kingine kilicho na uwezo mkubwa mno wa kuyakuza mawazo yetu, kuzipa nguvu fahamu za ubongo wetu, kama zilivyo hizo kweli pana, ziadilishazo, za Biblia. Kama wanadamu wangejifunza na kulichunguza Neno la Mungu kama inavyostahili, wangekuwa na maarifa mengi na tabia bora, na kuwa na kusudi thabiti ambalo katika nyakati hizi ni shida mno kuliona.
Lakini kuna manufaa kidogo tu yanayopatikana kwa kusoma Maandiko kwa haraka. Mmoja anaweza kuisoma Biblia yote, lakini bado ashindwe kutambua uzuri wake, wala kuelewa maana yake yenye kina iliyojificha. Kujifunza kifungu kimoja cha maneno mpaka maana yake imekuwa dhahiri, na uhusiano wake na mpango wa wokovu unaeleweka wazi, kuna manufaa mengi sana kuliko kuzisoma sura nyingi kwa juu juu tu bila ya kuwa na kusudi lo lote dhahiri wala kupata mafundisho yo yote yanayojenga.
Biblia yako iwe karibu nawe kila mara. Kila upatapo nafasi, isome; jifunze mafungu yake kwa moyo. Hata wakati utembeapo mitaani, waweza kusoma fungu fulani, na kwa njia hiyo kulikaza mawazoni mwako.Hatuwezi kupata hekima bila kujitahidi kwa dhati na kujifunza kwa moyo wa maombi. Baadhi ya sehemu za Maandiko maana yake imekuwa dhahiri kabisa; lakini kuna sehemu nyingine ambazo maana yake si rahisi kufahamika mara moja. Maandiko yanapaswa kulinganishwa na Maandiko mengine. Lazima pawe na utafiti wa makini na kutafakari kwa moyo wa maombi. Na kujifunza kama huko kutapata malipo maradufu. Kama vile mchimba madini anavyogundua mabamba ya mawe ya madini ya thamani yaliyojificha chini ya uso wa nchi, ndivyo yule anayestahimili kulichunguza Neno la Mungu, kama hazina iliyositirika, azionavyo kweli za thamani kuu mno, ambazo zimefichwa asiweze kuziona mtafutaji mzembe. Maneno hayo ya uvuvio, tukiyatafakari mioyoni mwetu, yatakuwa kama vijito vitiririkavyo kutoka katika chemchemi ya uzima.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)