Lebo

29/11/2014

ASOMAYE NA AFAHAMU

                    
Pombe haikuwa sehemu ya kinywaji ambacho Mungu alimpa
mwanadamu; maji safi na salama ndicho kinywaji bora kuliko
vyote kwa mwanadamu (Mithali 20:1; 23:29-35). Walevi
hawataurithi ufalme wa Mungu (1 Kor. 6:9,10; Gal. 5:21). Kuna
wengi wanaosema, "Mimi nakunywa sana, lakini silewi." Tatizo
la pombe sio kulewa tu, bali ni zile athari zinazotokana na
kunywa pombe ambayo ina sumu mbaya ya alkoholi. Sumu hiyo
huathiri vibaya moyo, mishipa ya fahamu, nyama za mwili na
kadhalika. Mungu atamharibu mtu ye yote anayeuharibu mwili wake
kwa makusudi kwa njia yo yote ile ----- pombe, tumbako, madawa
ya kulevya, na kadhalika (1 Kor. 3:16,17). Pia kuna vinywaji
vinavyopendwa na watu wengi aina ya 'Cola', Kahawa, na Majani ya
Chai ambavyo huidhuru mishipa ya fahamu, ubongo na mwili.
Viepukwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Tuandikie maoni yako hapa. Leave your comments here