Kamati Kuu ya Union ya Kusini mwa Tanzania ya Kanisa la Waadventista wa
Sabato, leo imefanya mabadiliko ya wakurugenzi ambapo Mchungaji Sadock
Butoke aliyekuwa Katibu Mkuu wa iliyokuwa Konferensi ya Mashariki mwa
Tanzania anakuwa Mkurugenzi wa Uwakili, Majengo, Shule ya Sabato na
Huduma binafsi wa Kusini mwa Tanzania, akichukua nafasi ya Rabson Nkoko
aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya ya Konferensi ya Nyanda za Juu
Kusini. Idara ya Mawasiliano sasa itashikwa na mchungaji Stephen Letta,
ambaye ataendelea kushika pia nafasi ya Katibu wa Wachungaji na
Mkurugenzi wa Huduma za Familia na VOP. Tuwaombee katika majukumu yao
haya mapya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Tuandikie maoni yako hapa. Leave your comments here