Lebo

19/04/2015

JE, WAFU WANAWEZA KUONGEA NASI?


Huduma ya malaika watakatifu, kama ilivyoelezwa katika Maandiko, ni ukweli wenye
faraja kuu na wa thamani kwa kila mfuasi wa Kristo.Walakini fundisho la Biblia juu ya jambo hili limetiwa giza na kupotoshwa kwa njia ya makosa yanayotokana na theolojia inayopendwa sana na watu wengi.

Fundisho lile lisemalo kwamba mwanadamu ana roho isiyokufa, ambalo liliazimwa kwanza kutoka kwa falsafa ya kipagani, na hatimaye wakati wa giza lile la UASI MKUU likaingizwa katika imani ya Kikristo, limechukua mahali pa ile kweli, inayofundishwa kwa wazi kabisa katika Maandiko, kwamba

 "WAFU HAWAJUI NENO LO LOTE." Watu wengi sana wamekuja kuamini kwamba ni roho za
wale waliokufa "watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu."
Walakini [imani] hiyo ni kinyume na ushuhuda wa Maandiko yanayohusu kuwako kwa
malaika mbinguni, na uhusiano wao na historia ya mwanadamu, kabla ya [kutokea] kifo
cha mwanadamu ye yote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Tuandikie maoni yako hapa. Leave your comments here