Basi mtiini Mungu.Mpingeni Shetani,naye atawakimbia Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi,na kuishafisha mioyo yenu,enyi wenye nia mbili{Yakobo 4:7-8} Submit yourselves then, to God, Resist the devil,and he will flee from you.come near to God and he will. come near you.wash your hands you sinners and purify your hearts you double minded.{James 4:7-8}NIV
14/07/2015
Jinsi Mungu Anavyompenda Mwanadamu- 2
Ingawa dunia imeanguka katika hali mbaya kwa ajili ya dhambi, lakini yote yaliyomo si huzuni na mashaka. Viumbe vya ulimwengu vimekuwa kama mitume waMungu kutuletea habari za faraja na utulivu. Kila mti wa miiba una maua yake pia; yaani, katika kila shida twaweza kupata baraka za Mungu.
“Mungu ni pendo” imeandikwa juu ya kila chipukizi, juu ya ncha ya kila jani dogo linalochipua. Ndege wazuri wanaoijaza anga na nyimbo zao za furaha, kila aina ya ua lililotiwa rangi nzuri katika ukamilifu wake likitia harufu yake nzuri katika hewa, miti mirefu sana ya msituni pamoja na majani yake mazuri ya kijani kilichokolea yote hutushuhudia upendo na utunzaji wa Mungu, jinsi anavyotaka kuwafurahisha watoto wake.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Tuandikie maoni yako hapa. Leave your comments here