Basi mtiini Mungu.Mpingeni Shetani,naye atawakimbia Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi,na kuishafisha mioyo yenu,enyi wenye nia mbili{Yakobo 4:7-8} Submit yourselves then, to God, Resist the devil,and he will flee from you.come near to God and he will. come near you.wash your hands you sinners and purify your hearts you double minded.{James 4:7-8}NIV
20/07/2015
KUTUBU
Sehemu ya 1
Je, mwanadamu anawezaje kuwa mwenye haki mbele za Mungu? Mwenye dhambi anawezaje kufanywa kuwa mwenye haki? Ni kwa njia pekee ya Kristo sisi tunaweza kupatanishwa na Mungu na kuwekwa katika hali ya utakatifu; lakini, je, twawezaje kufika kwake Kristo? Wengi wangali wakijiuliza swali lile lile kama walivyojiuliza watu wengi siku ile ya Pentekoste walipochomwa mioyo yao kwa ajili ya dhambi zao, na kulia, “Tutendeje?”
Neno la kwanza la jibu la Petro lilikuwa ni hili “Tubuni.” Mahali pengine pia alisema hivi, “Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe.” Matendo 2:38; 3:19. Kutubu kunajumuisha huzuni kwa ajili ya dhambi, na kugeuka kwenda mbali nayo. Hatutaikataa dhambi mpaka hapo tutakapoona ubaya wake ulivyo hasa; yaani, hapatakuwa na badiliko la kweli katika maisha yetu mpaka hapo tutakapogeuka katika mioyo yetu na kwenda mbali nayo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Tuandikie maoni yako hapa. Leave your comments here