Dhambi inapozifisha hisia za kiroho, mwenye dhambi hatambui kasoro alizo nazo katika tabia yake, wala hatambui ukubwa wa dhambi aliyoitenda; na kama hajisalimishi chini ya uwezo umhakikishiao dhambi wa Roho Mtakatifu, anabaki katika hali ya kuwa nusu kipofu kwa dhambi yake. Maungamo yake si ya kweli wala hayatolewi kwa dhati.
Kwa kila kosa analoungama anaongeza kutoa udhuru kwa ajili ya njia yake mbaya huku akijipongeza, akisema kwamba laiti mambo yasingalikuwa vile, asingekuwa amefanya kosa hili au lile, ambalo kwalo anakaripiwa.
Adamu na Hawa walipokwisha kula matunda yaliyokatazwa, walijaa haya na hofu kuu. Kwanza kabisa, walifikiri namna ya kujitetea kwa ajili ya kosa lao, ili waepukane na hukumu ya kifo waliyoiogopa sana. Bwana alipowauliza habari ya kosa lao, Adamu alijibu, huku kwa sehemu fulani akiliweka kosa lile juu ya Mungu na kwa sehemu juu ya mwenzi wake: “Mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala.” Yule mwanamke akamtupia lawama nyoka, akasema, “Nyoka alinidanganya, nikala.” Mwanzo 3:12,13. Kwa nini ulimwumba nyoka? Kwanini ulimruhusu aje katika Edeni? Haya ndiyo maswali yaliyojificha katika udhuru aliotoa kwa ajili ya dhambi yake, kwa njia hiyo akimshitaki Mungu kuwa anawajibika kwa anguko lao.
Roho ya kujihesabia haki mtu mwenyewe mwanzo wake ilitoka kwa yule baba wa uongo, nayo imedhihirishwa na wana na binti wote wa Adamu. Maungamo ya jinsi hii hayavuviwi na Roho wa Mungu, wala hayatakubaliwa na Mungu. Ungamo la kweli litamfanya mtu abebe dhambi yake mwenyewe, na kuiungama bila ya kuwa na udanganyifu au unafiki. Kama yule mtoza ushuru maskini, pasipo kuinua sana macho yake kuelekea mbinguni, atalia, akisema, “Mungu uniwie radhi mimi mwenye dhambi;” na wale wanaokiri dhambi zao watahesabiwa haki; kwa maana Yesu atawaombea akidai damu yake iliyomwagika kwa ajili ya mwenye dhambi atubuye.
Basi mtiini Mungu.Mpingeni Shetani,naye atawakimbia Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi,na kuishafisha mioyo yenu,enyi wenye nia mbili{Yakobo 4:7-8} Submit yourselves then, to God, Resist the devil,and he will flee from you.come near to God and he will. come near you.wash your hands you sinners and purify your hearts you double minded.{James 4:7-8}NIV
12/12/2015
07/12/2015
KUUNGAMA DHAMBI__3
Zamani wakati wa Samweli, Waisraeli walimwasi Mungu. Walikuwa wakiteseka kama matokeo ya dhambi zao; maana walikuwa wamepoteza imani yao kwa Mungu, walikuwa wamepoteza utambuzi wao kuhusu nguvu na hekima yake katika kulitawala taifa lile, walipoteza imani yao kuhusu uwezo wake wa kuwalinda na kuithibitisha kazi yake.
Wakampa kisogo Mfalme Mkuu wa Malimwengu, na kutamani kutawaliwa kama mataifa yale yaliyowazunguka. Kabla hawajaipata amani, walitoa ungamo hili halisi: “Tumeongeza dhambi zetu kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme.” 1 Sam. 12:19. Kosa lile lile hasa ambalo walitiwa hatiani lilipaswa kuungamwa. Kutokuwa na shukrani kwao kuliitesa mioyo yao, na kuwatenga mbali na Mungu.
Ungamo halitakubaliwa na Mungu bila ya kuwapo toba ya kweli na badiliko la maisha. Lazima badiliko dhahiri lionekane katika maisha ya mtu; kila kitu kimchukizacho Mungu ni lazima kiondolewe na kutupwa mbali. Hayo yatakuwa ndiyo matokeo ya huzuni ya kweli kwa ajili ya dhambi. Kazi ile tupaswayo kufanya kwa upande wetu imewekwa wazi mbele yetu: “Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya; jifunzeni kutenda mema;takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane.”
Isa. 1:16,17. “Kama mtu mwovu akirudisha rehani, na kumrudishia mtu mali yake aliyomnyang’anya, akizifuata sheria za uzima, asitende uovu wo wote; hakika ataishi, hatakufa.” Eze. 33:15. Paulo, akiongea juu ya kazi ya toba, asema hivi: “Maana angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.” 2 Kor. 7:11.
Wakampa kisogo Mfalme Mkuu wa Malimwengu, na kutamani kutawaliwa kama mataifa yale yaliyowazunguka. Kabla hawajaipata amani, walitoa ungamo hili halisi: “Tumeongeza dhambi zetu kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme.” 1 Sam. 12:19. Kosa lile lile hasa ambalo walitiwa hatiani lilipaswa kuungamwa. Kutokuwa na shukrani kwao kuliitesa mioyo yao, na kuwatenga mbali na Mungu.
Ungamo halitakubaliwa na Mungu bila ya kuwapo toba ya kweli na badiliko la maisha. Lazima badiliko dhahiri lionekane katika maisha ya mtu; kila kitu kimchukizacho Mungu ni lazima kiondolewe na kutupwa mbali. Hayo yatakuwa ndiyo matokeo ya huzuni ya kweli kwa ajili ya dhambi. Kazi ile tupaswayo kufanya kwa upande wetu imewekwa wazi mbele yetu: “Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya; jifunzeni kutenda mema;takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane.”
Isa. 1:16,17. “Kama mtu mwovu akirudisha rehani, na kumrudishia mtu mali yake aliyomnyang’anya, akizifuata sheria za uzima, asitende uovu wo wote; hakika ataishi, hatakufa.” Eze. 33:15. Paulo, akiongea juu ya kazi ya toba, asema hivi: “Maana angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.” 2 Kor. 7:11.
05/12/2015
KUUNGAMA DHAMBI__2
Wale ambao hawajajinyenyekeza mioyo yao mbele za Mungu na kuziungama dhambi zao, bado hawajalitimiza sharti la kwanza la kukubaliwa na Mungu. Kama hatujasikia toba lisilo na majuto (2 Kor. 7:10), wala hatujaziungama dhambi zetu kwa moyo wa unyenyekevu na uliovunjika, na kuyachukia maovu yetu, tutakuwa kweli hatujawahi kamwe kutafuta msamaha wa dhambi zetu; na kama hatujautafuta, basi hatujawahi kamwe kuipata amani ya Mungu. Sababu ya pekee kwa nini hatupati msamaha wa dhambi zetu zilizopita ni kwamba hatuko tayari kuinyenyekeza mioyo yetu
na kutimiza masharti ya neno la kweli.
Maagizo dhahiri yametolewa kuhusu suala hili. Ungamo la dhambi, liwe hadharani au faraghani, ni lazima litoke moyoni hasa, na litolewe kwa hiari. Mwenye dhambi asilazimishwe kutoa ungamo hilo. Wala halipaswi kutolewa kwa mzaha-mzaha tu au bila kujali, au kwa kuwalazimisha wale ambao hawana hisia yo yote juu ya hali mbaya mno ya kuchukiza ya dhambi.Ungamo lile litokalo moyoni hasa humfikia Mungu mwenye huruma isiyo na kikomo. Mtunga Zaburi asema,Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa.” Zaburi 34:18.
Ungamo la kweli daima ni la aina yake, nalo linakiri dhambi halisi zilizofanywa. Pengine ni dhambi ambazo imetupasa sisi kuzikiri kwa siri mbele za Mungu tu; pengine ni tendo baya ambalo linapaswa kuungamwa kwa mtu mmoja tu, yaani, yule aliyeathirika kutokana na tendo lile; au pengine ni kosa lililotendwa mbele ya watu lililowaumiza mioyo yao, ambalo linapaswa kuungamwa mbele yao. Lakini maungamo yote ni lazima yawe dhahiri na yakiri kosa lile lile hasa ulilolitenda.
na kutimiza masharti ya neno la kweli.
Maagizo dhahiri yametolewa kuhusu suala hili. Ungamo la dhambi, liwe hadharani au faraghani, ni lazima litoke moyoni hasa, na litolewe kwa hiari. Mwenye dhambi asilazimishwe kutoa ungamo hilo. Wala halipaswi kutolewa kwa mzaha-mzaha tu au bila kujali, au kwa kuwalazimisha wale ambao hawana hisia yo yote juu ya hali mbaya mno ya kuchukiza ya dhambi.Ungamo lile litokalo moyoni hasa humfikia Mungu mwenye huruma isiyo na kikomo. Mtunga Zaburi asema,Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa.” Zaburi 34:18.
Ungamo la kweli daima ni la aina yake, nalo linakiri dhambi halisi zilizofanywa. Pengine ni dhambi ambazo imetupasa sisi kuzikiri kwa siri mbele za Mungu tu; pengine ni tendo baya ambalo linapaswa kuungamwa kwa mtu mmoja tu, yaani, yule aliyeathirika kutokana na tendo lile; au pengine ni kosa lililotendwa mbele ya watu lililowaumiza mioyo yao, ambalo linapaswa kuungamwa mbele yao. Lakini maungamo yote ni lazima yawe dhahiri na yakiri kosa lile lile hasa ulilolitenda.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)