Lebo

17/08/2015

Waliopewa Kitabu - 3

Aya hizi ni NUKUU  kutoka DivineIslam’s Qur’an Viewer software v2.913

 

 Nukuu ili ishia hapa )

Watu hao wanasadiki kwamba ni jukumu lao kujitoa kabisa kwa Mwenyezi Mungu pasipo kuzuia kitu, kuwa na utii kwake usio na swali. Watu hao wana maadili ya kiwango cha juu, ambayo yamejengwa juu ya Maandiko ya Biblia.

 

ENDELEA HAPA 

Wanamheshimu Mwenyezi Mungu kuwa ndiye Mkuu kuliko wote, tena hawana mshirika ye yote (kama vile Maryamu au wale wengine waitwao watakatifu wanaoabudiwa) ambaye wanamfungamanisha na huyo Mungu kama Wakristo wengi sana wafanyavyo. Katika Injili maneno haya hunenwa: Yakobo 2:19 “Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema  na katika Marko (Isa al-Masih) Kristo Mwenyewe alisema… “Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja”. Watu hao hawazisujudu sanamu katika ibada yao kama wafanyavyo Wakristo wengi sana.

Wanasadiki kwamba kuabudu sanamu au mifano iwayo yote kumekatazwa kabisa na Mwenyezi Mungu, kama ilivyoandikwa katika Taurati, Kutoka 20:4-5 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala
mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia”. Watu hao wanajua kwamba kuabudu hiyo mifano na sanamu kumekatazwa kabisa katika Maandiko ya Biblia.


Yaendelea [Kurani Tukufu] kusema kwamba watu hao katika ibada yao kwa Mwenyezi Mungu ‘wanasujudu’, yaani, wanapiga magoti mbele zake Mwenyezi Mungu kama Daudi alivyoandika katika Zaburi (Taurati), Zaburi 95:6 “Njoni, tuabudu, tusujudu, tupige magoti mbele za
BWANA aliyetuumba.” Katika Sura 3:114 inatuambia sisi kwamba ‘wanakataza maovu’. ‘Hao’ miongoni mwa “wao Waliopewa Kitabu” wanakataza kula vyakula najisi (haramu) kama ‘Nyama ya
nguruwe’. (Taurati) Mambo ya Walawi 11:7 “Na nguruwe, … yeye ni najisi kwenu.” Wanakataza matumizi ya vileo, tumbako, na vitu vingine vinavyodhuru (haramu) afya ya mwili ambavyo vinauangamiza. Wanaziheshimu Amri Kumi za Mwenyezi Mungu kama zilivyoandikwa
katika (Taurati) Kutoka 20. Watu hao wanasadiki kwamba tunaishi katika “Siku za Mwisho” za historia ya dunia hii…

10/08/2015

Did you know the God’s Purpose for the Youth?????

A Call to the Youth _ PART 10

Make it the law of your life from which no temptation or side interest shall cause you to turn,Through Jesus Christ show that you are worthy of the sacred trust with which the Lord has honored you in bestowing upon you life and grace. You are to refuse to be in subjection to the power of evil. As soldiers of Christ we must deliberately and intelligently accept His terms of salvation under every circumstance, cherish right principles, and act upon them. Divine wisdom is to be a lamp to
your feet. Be true to yourselves, be true to your God.

Everything that can be shaken will be shaken; but rooted and grounded in the truth, you will abide with those things that cannot be shaken. The law of God is steadfast, unalterable; for it is the expression of the character of Jehovah. Make up your mind that you will not by word or influence cast the least dishonor upon its authority.

KUTUBU - 5

TUMEWEZA  KUONA Sala ya Daudi baada ya kuanguka kwake dhambini inatudhihirishia vizuri jinsi huzuni ya kweli kwa ajili ya dhambi ilivyo hasa. Kutubu kwake kulikuwa kwa kweli na kwenye kina. Kutubu kwa namna hii hakuwezekani kwetu sisi kwa uwezo wetu wenyewe; kunawezekana katika Kristo tu, aliyepaa juu na kuwapa wanadamu vipawa.

Hapo ndipo wengi wanapopotea, na hivyo hushindwa kupokea msaada anaotaka kuwapa Kristo. Wao wanadhani kwamba hawawezi kuja kwa Kristo isipokuwa kwanza wawe wamekwisha kutubia
dhambi zao, na ya kwamba kutubu kunawaandaa kupokea msamaha kwa ajili ya dhambi zao. Ni kweli kwamba kutubu kunakuja kabla ya msamaha wa dhambi; maana ni moyo ule tu uliovunjika na kupondeka, unaoona kwamba unamhitaji Mwokozi. Lakini je! ni lazima mwenye dhambi angoje mpaka amekwisha tubu kabla ya kwenda kwa Yesu? Je! toba iwe kizuizi kati ya mwenye dhambi na Mwokozi?


Katika Biblia, yaani, Neno la Mungu, hatusomi kwamba mwenye dhambi hana budi kutubu kabla ya kukubali mwito wa Kristo asemaye, “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.” Mt. 11:28. Ni uwezo unaotoka kwa Kristo unaowawezesha watu kutubu kweli kweli. Petro aliwaeleza Waisraeli mambo haya kwa dhahiri aliposema, “Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.” Mdo. 5:31.

Kadiri tusivyoweza kusamehewa dhambi bila Kristo, ndivyo tusivyoweza kutubu pasipo Roho wa Kristo kuziamsha dhamiri zetu. Kristo ndiye asili ya kila fikara njema. Yeye tu ndiye awezaye kupanda mbegu ya kuchukia dhambi katika moyo. Kila tamaa moyoni mwetu ya kutaka kuijua kweli na kuwa na maisha safi, kila kusadikishwa moyoni mwetu kunakotuonyesha kuwa sisi ni wenye dhambi, ni ushahidi uonyeshao kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi mioyoni mwetu.

Waliopewa Kitabu - 2

Aya hizi ni NUKUU  kutoka DivineIslam’s Qur’an Viewer software v2.913


Kurani Tukufu yasema hivi kuhusu kundi hilo la pekee, kwamba hao “ndio miongoni mwa hao watendao mema kweli kweli”. Iwapo hao ni miongoni mwa hao watendao mema kweli kweli, basi yale wayasadikiyo hayana budi kuwa ndiyo kweli yenyewe. Kama Mwenyezi Mungu anawaita kuwa wamo miongoni mwa hao watendao mema kweli kweli, basi, sisi hatuthubutu kabisa kuwakosoa.
Lakini je! si afadhali sisi pia tungeweza kujifunza kitu kwao?


Twaona ya kwamba watu hao wa pekee wanakishikilia kile ‘Kitabu’ (Maandiko ya Biblia) ambacho
Nabii Muhammad kwa makusudi mazima alituelekeza sisi kwenye [Kitabu] hicho katika Kurani Tukufu (Al Maidah) Sura 5:46 … “Na tukawafundisha (Mitume hiyo) Isa bin Maryamu
kuyahakikisha yaliyokuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uongozi na nuru na isadikishayo yaliyokuwa kabla yake katika Taurati, na uongozi na mauidha kwa wamchao (Mwenyezi Mungu).”

Watu hao wanasadiki kwamba ni jukumu lao kujitoa kabisa kwa Mwenyezi Mungu pasipo kuzuia kitu, kuwa na utii kwake usio na swali. Watu hao wana maadili ya kiwango cha juu, ambayo yamejengwa juu ya Maandiko ya Biblia.



09/08/2015

Did you know the God’s Purpose for the Youth?????

A Call to the Youth _ PART 9


Every student should understand that the principles which he adopts become a living, molding
influence upon character. He who accepts Christ as his personal Saviour, will love Jesus, and
all for whom Christ has died; for Christ will be in him a well of water springing up unto everlasting life. He will surrender himself without reservation to the rule of Christ.



Assert Your Liberty
Make it the law of your life from which no temptation or side interest shall cause you to turn, to honor God, because He “so loved the world, that He gave his only-begotten Son, that whosoever
Standards of Success believeth in Him should not perish, but have everlasting life.” As a redeemed, free moral agent, ransomed by an infinite price, God calls upon you to assert your liberty, and employ your God-given powers as a free subject of the kingdom of heaven. Be no longer under the thralldom of sin, but as a loyal subject to the King of kings, prove your loyalty to God.

08/08/2015

KUTUBU - 4


Sala ya Daudi baada ya kuanguka kwake dhambini inatudhihirishia vizuri jinsi huzuni ya kweli kwa ajili ya dhambi ilivyo hasa. Kutubu kwake kulikuwa kwa kweli na kwenye kina. Hapakuwa na
jitihada yo yote ya kupunguza ukubwa wa makosa yake; hakuwa na tamaa yo yote ya kuikwepa hukumu iliyotishiwa juu yake ambayo iliivuvia sala yake. Daudi aliuona ukubwa upitao kiasi wa kosa lake; aliona unajisi wa moyo wake; aliichukia sana dhambi yake. Hakuomba ili apate msamaha tu, aliomba pia ili awe na moyo safi. Alitamani sana kuwa na furaha iletwayo na utakatifu - yaani,
kurejeshwa katika hali ya amani na ushirika na Mungu. Hii ilikuwa ndiyo lugha ya roho
yake:


Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake.  Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila.” Zaburi 32:1-2. “Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu. Na dhambi yangu i mbele yangu daima Unioshe nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.

 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu. Usinitenge na uso wako, Wala Roho wako Mtakatifu usiniondolee. Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi, Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu, Utuponye na damu za watu Na ulimi wangu utaiimba haki yako.” Zaburi 51:1-14. Kutubu kwa namna hii hakuwezekani kwetu sisi kwa uwezo wetu wenyewe; kunawezekana katika Kristo tu, aliyepaa juu na kuwapa wanadamu vipawa.

Waliopewa Kitabu - 1

Aya hizi ni NUKUU  kutoka DivineIslam’s Qur’an Viewer software v2.913


Assalamu’ alaikum! Kurani Tukufu huelekeza kidole chake kwenye kundi lile liitwalo “Waliopewa Kitabu”. Msomaji anaombwa asome Sura 3:113-115. Aali Imran. 003:113 “Wao (Waliopewa Kitabu) si wote sawa. Katika (hao) Waliopewa Kitabu wamo watu waliotengenea  wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu (yaani wamesilimu).” 003:114 “Wanamwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na wanaamrisha mema na wanakataza maovu na wanayaendea mbio mambo mema.

Na hao ndio miongoni mwa hao watendao mema (kweli kweli).” 003:115 “Na heri yo yote watakayoifanya hawatakanushiwa (thawabu zake). Na Mwenyezi Mungu anawajua wanaomcha (wakajiepusha na makatazo yake na wakafanya maamrisho yake).” 


 Watu hao wanajulikana kama ‘Wakristo’. Hao wanaitwa ‘Waliopewa Kitabu’ (Maandiko ya Biblia). Lakini miongoni mwao limo kundi la pekee. Kurani Tukufu yasema kwamba ipo tofauti kati ya hao ‘Wakristo’ na ya kwamba ‘si wote sawa.’

Je, kundi hilo la pekee ni akina nani ambao Nabii Muhammad (jina lake na liheshimiwe) alivuta mawazo ya watu kuelekea kwao kwa namna ya ajabu kama hiyo, ya kuwa wao ni ‘miongoni mwa hao watendao mema kweli kweli’! Hebu zingatia tabia zinazolitambulisha kundi hili la pekee kutoka katika Sura 3:113-115
 

1. si (Wakristo) wote sawa
 

2. katika (hao) waliopewa Kitabu wamo watu waliotengenea
 

3. wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu
 

4. wanasujudu
 

5. wanamwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho
 

6. wanaamrisha mema [wanafundisha kwa mamlaka yaliyo ya haki]
 

7. wanakataza maovu
 

8. wanayaendea mbio mambo mema [wanajitahidi kufanya yale yenye sifa njema]
 

9. hao ndio miongoni mwa hao watendao mema kweli
kweli
 

10. na heri yo yote watakayoifanya hawatakanushiwa. [Mwenyezi Mungu anawajua]